SIKU YA WAKAGULU DAR ES SALAAM
Mabadiliko ya Tamasha la Wakagulu Mkoa wa Dar es Salaam lililokuwa lifanyike Kijiji Cha Makumbusho Kijitonyama Sasa limehamishiwa Maeneo ya Chang'ombe GWAMBINA LOUNGE Zamani palijulikana kama TTC.
Wadau turejee kwenye kuhakikisha SAFARI YA MKAGULU TANZANIA tunashiriki kikamilifu kwasababu ni waalikwa rasmi kwenye Tamasha hilo.
Kuna gharama za kupeleka Zana zote za Kikagulu kutoka Gairo kwenda DSM kwa ajili ya Maonyesho haya yatakayo weka Historia na kuhudhuriwa na wageni wengi pamoja na Viongozi wetu wa Serikali.
Shime shime tuwape nguvu Viongozi wetu kwa Kuhakikisha gharama ndogondogo za kufanikisha jambo hili linafanikiwa tunayo Imani Wakaguru mtaguswa na hili na kuwakilisha michango yenu kwa Viongozi.
Kama kuna mwenye moyo wa kutoa na hapendi aonekane hapa basi karibu kwa Mchango wako tufanikishe jambo hili muhimu kwetu.
Kwa Ufafanuzi zaidi piga simu Namba 0716679398 AFISA HABARI NA MAWASILIANO SAFARI YA MKAGULU TANZANIA Ndg. Mndewa Chitiligiti ✍ JM.
MWENYEZI MUNGU AWABARIKI NA KUWAGUSA KATIKA HILI WANA WA SAFARI YA MKAGURU.
No comments:
Post a Comment