PAGES

Monday, April 12, 2021

HISTORIA YA WAKAGULU


HISTORIA, MILA NA DESTURI ZA WAKAGULU

Wakagulu ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Morogoro, Wilaya ya Kilosa. Lugha yao ni Kikagulu. Wakagulu ni mojawapo ya makabila makubwa katika mkoa wa Morogoro, Wakagulu zaidi wapo katika Wilaya za Kilosa, Gairo, Mpwapwa, Kongwa, Kiteto na sasa wanatanuka zaidi maeneo ya handeni. Ukifuatilia Simulizi za wazee, hususani wakati wa sherehe za kumaliza msiba (mwidiki) inaonesha kuwa Wakagulu walitokea maeneo ya Rwanda na Burundi (yasasa). Walitoka maeneo hayo kutokana na ukame uliokuwepo na matatizo mengine ya kivita. Walipita maeneo mengi yakiwemo KONONGO (UKIMBU) Mkoani Rukwa baadaye walipita maeneo ya Mkoa wa Singida hadi wakaingia RUDI (KUSINI MWA MPWAPWA). Baada ya kuishi hapo kwa muda waliparamia milima ya Lubeho, lakini bado walikuwa na mawasiliano makubwa na watu wa Konongo. Katika kuzunguuka hapa na pale huko milimani ndipo zilipojitokeza Koo mbalimbali za wakagulu kutokana na matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiwapata wanawake. Kwa msingi huo Wakagulu wanachukua ukoo kutoka kwa mama (Welekwa). Kwa mfano ukoo wa Wambigo ulipatikana baada ya wahenga kukanyaga maji yaliyokuwa yanajizunguusha (Gakubiga) kwenye mto Mkondoa  na Ukoo wa Wanjeja wao walipata jina la ukoo wao baada ya kufanya safari ndefu na ulipofika usiku walienda kulala kwenye mti unaoitwa MNJEJA. Hao ndio Wakagulu. 





No comments:

Post a Comment

UTALII UKAGULUNI UMESHAFUNGULIWA TWENDENI TUKATALII WILAYA YA KILOSA NA GAIRO MKOANI MOROGORO.

 PICHA KATIKA MATUKIO YA UTALII UKAGULUNI. Wilaya ya Kilosa na Gairo zilizopo Mkoani Morogoro zimebarikiwa kuwa na vivutio vingi sana ambavy...